Dar es salaam 28-01-2022
Shirika la viwango Tanzania(TBS) linapenda kuwakubusha mawakala na waagiza wa bidhaa za chakula na vipodozi nje ya nchi kuhakikisha wanasajili bidhaa za chakula na vipodozi kabla ya kuziingiza nchini ili kuendana na takwa la sheria ya viwango ya mwaka 2009 pamoja na kanuni ya udhibiti ubora wa shehena ya mwaka 2021 “The standards(Import registration and Batch Certification) Regulations GN.681 of 2021” ambayo inamtaka kila muagizaji ni lazima kusajili kwanza bidhaa za chakula na vipodozi kabla ya kuziingiza nchini.
Hivyo basi ili kuepuka usumbufu na gharama ni vema waagizaji wakasajili bidhaa hizo kabla ya kuiingiza nchini kuendana na matakwa ya kisheria.
Kwa maelezo zaidi piga namba ya bure 0800110827.
Imetolewa na:
Gladness H Kaseka
Mkuu wa kitengo cha Uhusiano na Masko
Shirika la viwango Tanzania
DC Jokate Mwegelo Azindua Rasmi Tuzo Za Wajasiriamali Wa Twcc Jijini Dar
Read MoreWaziri Bashe Atangaza Sikukuu Ya Wakulima Nane Nane Kufanyika Mwaka Huu Wa 2022
Read MoreRaisi Samia Kuwa Mgeni Rasmi Siku Ya Maalum Ya Tanzania Kwenye Maonyesho Ya Expo Dubai 2020
Read More