Tanzania Women Chamber of Commerce

PROGRAM YA KUWEZESHA WANAWAKE NA VIJANA KUSHIRIKI MANUNUZI YA UMMA (BID FOR SUCCESS (B4S)- COHORT 4

Programu ya Bid for Success (B4S) kwa ajili ya kuwawezesha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu kwenye manunuzi ya umma inarejea tena! Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) kinayo furaha kutangaza awamu ya nne ya mafunzo maalum kwa vijana kutoka Dar es Salaam na mikoa ya yote Tanzania.

Mafunzo haya yanalenga kuwapatia washiriki ujuzi na maarifa muhimu ili waweze kushiriki kwa ufanisi katika mchakato wa manunuzi ya umma. Usikose fursa hii adhimu ya kuboresha uwezo wako kupitia programu ya B4S!
šŸ“MAFUNZO YATAFANYIKA MKOA WA DAR ES SALAAM

Lengo la Mafunzo

ā–¶ļøKuwajengea uwezo vijana kupanua wigo wa soko kupitia tenda za serikali na sekta binafsi.

ā–¶ļøKuongeza ushiriki wa vijana kwenye Fursa za manunuzi ya Umma

āœ…Vigezo vya kushiriki
1. Biashara yako iwe imesajiliwa ( uwe na TIN, na Leseni ya Biashara)

2. Biashara iwe inamilikiwa na kijana kwa asilimia 51 au zaidi

3. Biashara ilio tayari kukua na yenye mipango thabiti

4. ā Mjasiriamali au kampuni ambayo ina nia ya dhati ya kushiriki fursa za manunuzi ya umma kwenye Taasisi za serikali na kwenye sekta binafsi.

āœ…Faida ya Kushiriki
1. Kupata elimu ya kina na ya kitaalam kuhusu masuala ya tenda na michakato ya kushiriki manunuzi ya umma
2. ā kufahamishwa kuhusu fursa mbalimbali za zabuni
3. ā kujengewa uwezo wa kukuza na kumiliki biashara endelevu
4. ā Kuunganishwa, kuwezeshwa na kusajiliwa kwenye mifumo ya kidigitali kwa ajili ya kuona fursa mbalimbali za tenda zinazotangazwa ukiwemo mfumo wa serikali wa manunuzi ya Umma (NeST), mifumo ya UN, Sekta binafsi. N.k
5 Kuweza kuunganishwa na Mlezi mtaalamu/Mentors atakaekuongoza kwenye mchakato wako wa kushiriki fursa za zabuni
6. ā Fursa ya kuongozwa kuweza kuandaa mpango biashara
7. ā Kusaidiwa kutengeneza profile nzuri ya kampuni
8. Kuunganishwa na taasisi za fedha pale unaposhinda tenda ili kuweza kutoa huduma husika

Mwisho wa kutuma Maombi kwa washiriki wa awamu ya NNE ni tarehe 31 January, 2025

Ili kuweza kushiriki, Jaza fomu hii https://forms.gle/eTajuaAfReMoDYN38

Related Articles

Tanzania Women Chamber of Commerce | 12-07-2022

RAIS MWINYI AWAPONGEZA WAJASIRIAMALI WA TWCC

Read More
Tanzania Women Chamber of Commerce | 11-09-2022

TWCC WOMEN IN BUSINESS BREAKFAST MEETING 10 SEPTEMBA 2022

Read More
Tanzania Women Chamber of Commerce | 11-09-2022

ZIARA YA WANAWAKE NCHINI UTURUKI KUANZIA TAREHE 11-19 OKTOBA, 2022

Read More