Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) kinayo furaha kutangaza awamu ya nne ya Bid for Success (B4S), programu ya kipekee inayolenga kuwawezesha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika mchakato wa manunuzi ya umma. Programu hii maalum itafanyika katika Mkoa wa Mbeya, ikilenga mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.
Programu ya B4S inalenga kuwapatia washiriki maarifa na ujuzi muhimu ili kushiriki kwa ufanisi katika zabuni na tenda za serikali na sekta binafsi. Hii ni fursa adhimu ya kujijengea uwezo wa kukuza biashara yako na kushiriki katika soko pana.
Mwisho wa kutuma maombi kwa awamu ya nne ni Disemba 30, 2024.
Wajisajili wanahimizwa kujaza fomu kupitia kiungo hiki:
https://forms.gle/5uCBhSjq478r4fnHA
Usikose nafasi hii ya kipekee ya kuboresha biashara yako na kufungua milango mipya ya fursa!
RAIS MWINYI AWAPONGEZA WAJASIRIAMALI WA TWCC
Read MoreTWCC WOMEN IN BUSINESS BREAKFAST MEETING 10 SEPTEMBA 2022
Read MoreZIARA YA WANAWAKE NCHINI UTURUKI KUANZIA TAREHE 11-19 OKTOBA, 2022
Read More